Sunday, April 25, 2010

Simba Sc Wawafunga El Hadoud

Timu ya simba pichani iliyowafunga wamisri Haras Al Hadoud mabao 2-1 katika Uwanja wa taifa leo hii.Mabao ya Simba yalifungwa na Mgosi na Okwi.

Thursday, April 22, 2010

BINTI WA KITANZANIA APOTEA

Toronto Police Service News Release
Missing woman Elizabeth Chirwa, 22

Wednesday, April 21, 2010 - 12:18 PM 33 Division 416-808-3300

The Toronto Police Service is requesting the public's assistance locating a missing woman.

Elizabeth Chirwa, 22, was last seen on Tuesday, April 20, 2010, at 6:30 a.m., in the area of Graydon Hall Drive.

She is described as black, 5'3", 141 lbs, with straight, black hair in a ponytail. She may be carrying a small, black handbag.

Police are concerned for her safety.

Anyone with information is asked to contact police at 416-808-3300, Crime Stoppers anonymously at 416-222-TIPS (8477), online at www.222tips.com, or text TOR and your message to CRIMES (274637).

Constable Isabelle Cotton, Public Information, for Detective Brian Martell, 33 Division

Washiriki wa Miss Universe Tanzania 2010

Tabia toka Dodoma Selina toka Dar Sanje toka Dodoma Redempta toka Moro Rose toka Dodoma Neema Nasra toka Dar Mwajabu toka Mwanza Maureen toka Moro Mary toka Moro Josephine toka Dar Immaculata toka Mwanza Halima toka Arusha Fatma toka Dar Gaudencia toka Moro Esther toka Mwanza Devota toka Dar Demitria toka Dar Anna toka Dar Hellen toka Arusha- ameibuka mshindi wa Miss universe Tanzania

Wednesday, April 21, 2010

Mbunge wa Wawi Pemba na Kiongozi wa upinzani katika bunge la Tanzania Mh. Hamad Rashid, alikutana na watanzania waishio katika jiji la Toronto na vitongoji vyake.Mkutano huo ulifanyika jumamosi ya terehe 17 ambapo mheshimiwa Hamad alipata fursa ya kusalimiana na kubadilishana mawazo ikiwa pamoja na kujibu maswali.
Kama ilivyo kwa viongozi wengine waliomtangulia Mheshimiwa alisisitiza umuhimu wa wazawa wa Tanzania kurudi nyumbani kuwekeza, alisema kuwa anafahamu kwamba bado kuna vikwazo lakini tusikate tamaa. Akitoa mfano alisema, yeye ameshafungua biashara ya uvuvi, usafiri wa anga bila mafanikio makubwa lakini bado hajakata tamaa.
Akijibu maswali Mheshimiwa alisema suala la uraia wa nchi mbili lipo katika hatua za mwisho kwani hata mipaka ya jumuia ya Afrika mashariki itafunguliwa mwakani (2011), vilevile akijibu tuhuma kuwa yeye amenunuliwa na chama tawala (CCM) alisema tuhuma hizo si za kweli na yeye alikuwa mtu wa kwanza kuzungumzia na kukemea tuhuma zilizohusisha mikataba mibovu.
Mwisho alisisitia kuwa yeye ni mtu safi ila huwa hapendi kukabiliana na matatizo kwa njia ya ugomvi, kashfa au matusi.Alimalizia kwa kusema baba yake aliwahi kumwambia kuwa kama mtu akimtuhumu kwa uchawi wakati si kweli basi hana sababu ya kuogopa.
Mheshimiwa Hamad Rashid alisafiri baadeye jioni kuendelea na ziara yake kuelekea BC.

TANESCO KUONGEZA MTANDAO WA UMEME MBINGA

Naibu Waziri wa Nishati na Madini Adam Malima akiongea na waandishi wa habari. Benjamin Sawe: Maelezo Dodoma Wizara ya Nishati na Madini kupitia Shirika la umeme nchini imepanga kuongeza mtandao wa umeme mjini Mbinga kwa kujenga ujenzi wa njia ya kilometa moja ya msongo wa KV 11. Naibu Waziri wa Nishati na Madini Adam Malima alisema ingawa Mbinga imeshapata umeme wa jenereta mbili zenye uwezo wa kuzalisha jumla ya MW2.5 bado kunahitajika umeme zaidi kulingana na shughuli za kiuchumi na jamii kuwa juu Alisema Tanesco pia itafunga transoma yenye uwezo wa KVA 100 ikiwa ni pamoja na kujenga njia ndogo ya umeme yenye urefu wa kilometa 2.0 ili kusambaza umeme maeneo ya Matika Tanki la maji mjini Mbinga. Kwa mujibu wa Mheshimiwa Malima pia itafungwa transofoma yenye uwezo wa KVA 100 na kujenga njia ndogo ya umeme yenye urefu wa kilometa 2.0 ili kusambaza umeme katika maeneo ya Matarawe Ruhuwiko Aidha Mheshimiwa Malima alisema Serikali itajenga njia ndogo ya umeme yenye urefu wa kilometa 1.5 ili kusambaza umeme maeneo ya kiwandani Mbambi. Alisema tatizo linalokwamisha upelekaji wa maeneo ya Maguu,Litembo,Matiri na Ruanda ni uwezo mdogo wa Serikali wa kutekeleza miradi ya kusambaza umeme nchi yote kwa pamoja kulingana na uwezo wa fedha. Hivyo amewahakikishia wananchi kwamba Serikali itaendelea na juhudi za kutafuta fedha za kufikisha umeme kwa viwango bora zaidi katika vijiji vya Maguu Litembo,Matiri na Ruanda kuliko ilivyo hivi sasa

Tuesday, April 20, 2010

HARAMBEE YA MAZISHI YA EVALINE

Ndugu, jamaa na marafiki wa Evaline katika maombi.

SHUKURANI

Familia ya Mzee Gembe wa Upanga Dar-es-salaam na Tabora,kwa moyo mkunjufu, tunapenda kuchukua nafasi hii kuwashukuru ndugu,jamaa,majirani na marafiki wote waliofanikisha shughuli zote za msiba wa Marehemu mtoto wetu,mdogo wetu,dada yetu, Evaline Gembe ambaye alifariki huko Toronto nchini Canada katika hospitali ya Mtakatifu Michael tarehe 30/March/2010 na hatimaye kuzikwa tarehe 13/Aprili/2010 kijijini Inyonga Mkoa wa Tabora.

Shukrani za pekee tunaomba ziwafikie Jumuiya yote ya watanzania wanaoishi nchini Canada hususani katika Jiji la Toronto na vitongoji vyake. Asanteni sana kwa michango yenu ya hali na mali ambayo ilisaidia katika mipango na mikakati yote ya kuuhifadhi mwili hadi kuusafirisha kwa gharama kubwa kutoka Toronto hadi Dar-es-salaam mnamo tarehe 8/April/2010.Asanteni kwa sala,maombi na kujitokeza kwenu katika kutufariji na kututia nguvu.Shukrani za pekee ziwaendee kamati nzima iliyoratibu na kufanikisha shughuli nzima ya kuusafirisha mwili wa Marehemu Evaline kuja Tanzania.

Tunapenda pia kutoa shukrani nyingi kwa majirani,ndugu,jamaa na marafiki kwa misaada yenu ya hali na mali na pia kushiriki katika shughuli zote za mazishi. Shukrani kwa wote mliofika nyumbani Dar-es-salaam na Tabora katika kutufariji,mliotupigia simu au kutuma ujumbe kwa njia zingine kwa nia ya kutufariji na kututia nguvu.Asanteni sana.

Shukrani pia ziuendee Ubalozi wa Tanzania nchini Canada na Jumuiya mbalimbali za ki-Tanzania nchini Marekani na wanablogu wote waliolitoa tangazo la kifo kwenye Blogu zao.

Kwa kuwa ni vigumu kumshukuru kila mtu kipekee,tunaomba shukrani hizi mzipokee wote mliohusika kwa njia moja ama nyingine katika kufanikisha shughuli nzima ya msiba huu wa ndugu yetu Evaline.Hatuna cha kuwalipa bali tunamwomba Mwenyezi Mungu awajalie na kuwazidishia katika shughuli zenu za kila siku.

Sisi tulimpenda sana Evaline lakini

Mwenyezi Mungu amempenda zaidi,

Jina la Bwana lihimidiwe.

Amen