Saturday, February 19, 2011

Msaada kwa walioathirika na Milipuko Gongo la mboto, Dar es salaam.

My friends and colleagues back home Pamela Lwakabare, Nancy Mwanyika, Tamika C Zaun, Aysha Mbarak, Babbie Kabae, just to name few. Have been on a movement gathering good, initiating people to donate blood and visiting affected area. As per report they have been able to get over 100 people to donate blood, today they were at Gongolamboto distributing mosquito nets donated, bedsheets donated by hotels and some perishable foods.
There's still need for these iteams and more.

In my family we are planning to send a little donation to support these ladies self initiated support program.
If you are interested in helping out please email me at scperr@rogers.com
A toonie or two hundred, anything will be appreciated.
I will be at TCA party tonight you're welcome to give me your donation there.
Please give me your email address with your donation to get details on how much was collected.

I will be collecting over this long weekend and send out all the money on Tuesday by Money gram.

I thank you all for your time in reading this Message.
Mungu ibariki Tanzania yetu.

Sarah Chuma-Perrin

Thursday, February 17, 2011

RAMBIRAMBI

 
RAMBIRAMBI
 
Kwa niaba ya Tanzanian Canadian Association (TCA), chama cha jumuiya ya Watanzania tunaoishi Toronto , Ontario , Canada na vitongoji vyake, tunapenda kuchukua fursa hii kwanza kabisa, kutoa rambirambi zetu kwa familia za wananchi waliopoteza wapendwa wao katika ajali ya mabomu yaliyolipuka katika kambi ya jeshi eneo la Gongo La Mboto, Dar-es- Salaam , Tanzania .
 
Tunawaombea wote waliopoteza maisha yao Mwenyezi Mungu awapumzishe kwa amani; tunawatakia majeruhi waugue pole, wapone haraka ili waweze kuendelea na shughuli zao za kila siku. Vilevile, tunawatakia wote waliopotezana na ndugu zao hususan watoto waliopotezana na wazazi wao waweze kupatikana na kukutana tena.
 
Tumesikitishwa na taarifa za maafa hayo na kuhuzunishwa kuona kwamba ni mara ya pili tukio kama hili linatokea nchini kwetu. Wengi watakumbuka siku si nyingi janga kama hili lilitokea kule Mbagala. Tunapenda kuuomba uongozi wa jeshi uangalie upya namna silaha kali zinavyohifadhiwa; katika utaratibu wa kuhifadhi mabomu, tunapendekeza yafanyike marejeo na marekebisho yatakayozingatia usalama wa raia.
 
Katika kuhitimisha, tunalisisitizia Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), lichukue hatua madhubuti na za haraka katika kuhakikisha majanga yanayoweza kuepukika kama haya hayatokei tena.
 
Mungu Ibariki Tanzania .
 
Uongozi – Tanzanian Canadian Association (TCA)